Rapa Dr. Dre anadaiwa kulazwa ICU katika Kituo cha Matibabu cha Cedars Sinai huko Los Angeles baada ya kuugua ugonjwa wa aneurysm ya ubongo
Vyanzo vinaeleza Dre alipata ugonjwa wa aneurysm Jumatatu na alikimbizwa na gari la wagonjwa kwenda Cedars na kupelekwa moja kwa moja ICU,
Nguli huyo wa muziki wa Rap mwenye umri wa miaka 55 Asubuhi ya leo amewatoa hofu mashabiki zake nakusema kwa sasa anaendelea vizuri
"Asante kwa familia yangu, marafiki na mashabiki kwa kuguswa na Kuniombea. Ninaendelea vizuri na ninapewa huduma bora na kwa timu yangu ya matibabu. Nitatoka hospitalini na kurudi nyumbani hivi karibuni. Niwashukuru Madaktari wote hapa Cedars, One Love !!" - Ameandika @Dr.dre kipitia ukurasa wake wa Instagram Asubuhi leo.
Rapa Dr. Dre alazwa ICU, awatoa hofu mashabiki zake
Reviewed by cmakigo
on
January 06, 2021
Rating:
Reviewed by cmakigo
on
January 06, 2021
Rating:

No comments:
Post a Comment